
Frank Arnesen ametoa angalizo hilo, baada ya kikosi cha klabu hiyo inachoshiriki ligi kuu ya soka nchini Ujerumani, kuwa chini ya meneja wa muda Rodolfo Cardoso ambae amekua akiifanya kazi hiyo bila ya kuwa na sifa zinazohitajiwa na shirikisho la soka barani ulaya UEFA.
Rodolfo Cardoso ameifanya kazi hiyo kwa muda wa mwezi mmoja, na hii ilikuja baada ya kuondoka kwa meneja Michael Oenning alishindwa kutimiza malengo ya klabu.

Lakini pamoja na mipango hiyo kuvurugika yasemekana uongozi wa Hamburg SV unajipanga kuzungumza na mchezaji wa zamani wa klabu hiyo Sergei Barbarez ambae ameonyesha nia ya kuwa tayari kuyavaa majukumu ya umeneja huko Imtech Arena.
No comments:
Post a Comment