KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Tuesday, October 4, 2011

PSG WAJIPANGA KUMSAJILI TEVEZ.

Ikiwa imepita siku moja baada ya kufanya mazungumzo na uongozi wa klabu ya Man City, mshambuliaji kutoka nchini Argentina Carlos Tevez, anahUsishwa na taarifa za kuwa mbini kuondoka klabuni hapo na kusajiliwa na vibopa wa ligi ya nchini Ufaransa Paris Saint-Germain.

Mkurugenzi wa ufundi wa PSG Leonardo Nascimento De Araujo amenukuliwa katika mtandao wa klabu hiyo akisema wanatazama uwezekano wa kutuma ofa ya kutaka kumsajili Carlos Tevez, kitakapofika kipindi cha usajili wa dirisha dogo mwezi januari mwakA 2012.

Amesema wanatambua kwa sasa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27, ana matatizo makubwa ya uongozi wa Man City hivyo wanatumia nafasi hiyo kutaka kumaliza mzozo unaoendelea huko Etihad Stadium kwa muda wa juma moja sasa.

Amesema kwamba Carlos Tevez, bado ana uwezo mkubwa wa kucheza soka na anaamini atakapobadilisha mazingira, atakuwa na uhuru wa kufanya makubwa zaidi hivyo wanasubiri na kutazama uwezekano wa kumsajili mwezi januari endapo mipango yao itakwenda kama wanavyotarajia.

Mbali na klabu ya PSG, pia klabu inayochipukia kwa kasi kubwa huko nchini Urusi ya Anzhi Makhachkala inahusishwa na taarifa za kutaka kumsajili Carlos Tevez huku klabu yake ya zamani wa West Ham Utd ikiondolewa katika utaratibu huo baada ya viongozi wa Man City kutupilia mbali taarifa zilizotolewa na mmoja wa wamili wa klabu hiyo ya magharibi wa mji wa London.

No comments:

Post a Comment