
mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23 tayari ameshatemwa katika kikosi ambacho kilichoitwa na kocha mkuu Samson Siasia aliepania kuipelekea timu ya taifa ya Nigeria katika fainali hizo ambazo zitachezwa nchini Gabon pamoja na Equatorial Guinea.
Victor Anichebe amesema ni wakati mgumu sana kwake kwa hivi sasa kufikiria ni vipi alivyokua anahitajika katika kikosi cha Super Eagles ambacho kitatakiwa kupata ushindi katika mchezo huo dhidi ya Guinea ili kujihakikishia nafasi ya kuwa miongoni mwa mataifa 16 ya barani Afrika yatakayoshiriki hapo mwakani.
Anichebe alipatwa na maumivu ya nyonga katika mchezo dhidi ya Madagascar uliochezwa mwezi uliopita, ambapo katika mchezo huo alichezeshwa kama mshambuliaji pekee, baada ya kocha Samson Siasia kuamua kutumia mfumo wa 4-2-3-1.
Hata hivyo bado mshambuliaji huyo ataendelea kuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi miwili ijayo, kufuatia majibu ya vipimo alivyofanyiwa siku za hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment