
Roman Abramovich alikua na matarajio ya kuuendeleza uwanja wa Stamforde Bridge kwa kuubomoa na kuutengeneza upya lakini utaratibu huo umepiga hatua na kufikiria kununua sehemu nyingine kwa ajili ya kujenga uwanja mpya ambao utakua chachu ya kupata makazi mapya ya klabu hiyo.
Tayari kibopa huyo ameshanunua sehemu ambayo ni karibu wa uwanja wa sasa, na endapo dhana ya kujenga uwanja mpya itakamilika basi Chelsea wataingai kati utaratibu wa kuwa miongoni mwa vilabu vitakavyomiliki uwanja utakaokuwa na uwezo wa kuchukua mashabiki elfu 60.
Hata hivyo ifahamike kwamba kwa sasa Roman Abramovich hana sauti ya umiliki wa uwanja wa Stamford Bridge, zaidi ya kuomba namna ya kununua hisa kutoka kwa mashabiki wa Chelsea wenye haki ya umiliki baada ya kufanya maboresho miaka 14 iliyopita.

Kwa upande wa mwenyekiti wa klabu hiyo Bruce Buck amesema ana imani wanahisa wa Chelsea watakubaliana na andiko hilo la Roman Abramovich.