Kiungo wa kimataifa toka jamuhuri ya Czech TOMAS ROSICKY amesema umefika wakati wa kulipa fadhila kwa mashabiki wa klabu ya Arsenal ambao walimsubiri kwa muda wa miezi 18 aliyokuwa nje akiuguza majereha yake ya goti pamoja na nyonga. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka, 28, amesema mashabiki wa klabu ya Arsenal, ni kweli walikuwa na hamu ya kumuona akirejea tena uwanjani, huku wakiwa na machungu ya kukosa usaidizi wake katika kikosi cha The Gunners hivyo halitokuwa jambo la busara endapo atashindwa kuwatimizia waliyokuwa wakiyasubiri toka kwake.
Aidha TOMAS ROSICKY amezungumzia juu ya hatua ya klabu yake kuwa
kwenye wakati mgumu wa kutwaa mataji kwa muda wa msimu kadhaa hivi sasa, ambapo amebainisha wazi kwamba hatua hiyo jibu lake litapatikana hivi karibuni na The Gunners ulimwenguni kote watafurahi kama ilivyo kwa mashabiki wa vilabu vingine.
kwenye wakati mgumu wa kutwaa mataji kwa muda wa msimu kadhaa hivi sasa, ambapo amebainisha wazi kwamba hatua hiyo jibu lake litapatikana hivi karibuni na The Gunners ulimwenguni kote watafurahi kama ilivyo kwa mashabiki wa vilabu vingine.Siku mbili zilizopita nahodha wa klabu ya Arsenal Francis Fabregas alizungumza na televisheni ya klabu hiyo na kueleza wazi juu ya kurejea kwa Rosicky.
Fabregas amesema anaamini kurejea kwa kiungo huyo kutasaidia kuleta nguvu ndani kikosi chao ambacho kinatarajia kufanya mabadiliko ya kiushindani msimu ujao.
Katika hatua nyingine beki wa kimataifa toka nchini Ubelgiji Thomas Vamalen ambae amesajili wa klabu hiyo akitokea Ajax Asterdam nae amezungumzia hatua ya kufurahishwa kwake na kujiunga na klabu hiyo.
Beki huyo mwenye umri wa miaka 23 amesema ni bahati ilioje kwake kusajiliwa na klabu kubwa kama Arsenal hivyo ni jukumu kwake kuhakikisha anacheza soka ambalo litaiwezesha klabu hiyo kubadilika kimtazamo inapokuwa uwanjani na nje ya uwanja.

Hata hivyo beki huyo amezungumzia juu ya upinzani ambao upo katika kikosi cha kwanza kwa kusema kwamba anaifahamu fika hali hiyo na kutambua kuwa nafasi anayocheza ina wachezaji wengi na wenye uwezo hivyo ni jukumu lake kujituma ipasavyo.




Meneja wa klabu ya Barcelona Pep Guardiola, ameliorodhesha jina la mshambuliaji wa kimataifa toka nchini Cameroon Samuel Eto'o katika orodha ya wachezaji atrakaowauza katika kipindi hiki cha usajili.








Hata hivyo amesema atakuwa tayari kutumia ada ya uhamisho wa Adebayor iwapo atampata mchezaji alie na umakini mkubwa na mwenye uwezo wa kuisadia Arsenal katika michuano kadha wa kadha msimu ujao.






















Hata hivyo kiungo huyo ameongeza kuwa angependa kurejea tena nchini Italia baada ya kuichezea kwa mkopo klabu ya AC Milan msimu uliopita.




